Showing posts with label Chadema. Show all posts
Showing posts with label Chadema. Show all posts
Saturday, September 28, 2013
End of the Year BBQ Party in Reading!
CHADEMA UK inawakaribisha waTanzania na wapenzi wote wa CHADEMA kwenye barbeque (End of the Year BBQ) party itakayofanyika Comunity Hall/Back Garden, 44 Watlington street, RG1 4RJ Reading tarehe 05-10-2013.
Mgeni rasmi atakuwa ni mwanasiasa mwenye kipaji cha pekee na muhimili muhimu wa CHADEMA – katibu wa CHADEMA Arusha na kanda ya kaskazini ndugu Amani Golugwa.
Itakuwa ni siku nzuri kujiburudisha kwa nyama choma, vinywaji na muziki free of charge. Lengo ni kuwakutanisha wapenda maendeleo katika kubadilishana mawazo na kujumuika katika harakati za kimaendeleo kwa taifa.
Hii shughuli si kwa wanaCHADEMA peke yake. Kila mTanzania mpenda maendeleo anakaribishwa kuhudhuria. Ni wakati mzuri kukaa pamoja tukijiburudisha huku tukibadilishana mawazo on party lines kiutu uzima bila malumbano. Wakati ni huu kuonesha utashi na ukomavu wa kisiasa.
Chakula na vinywaji bure!!!
Karibuni wote
Tuesday, June 18, 2013
CHADEMA UK YAMWANDIKIA BARUA RAISI. PIA YATUMA TAARIFA KWENYE TAASISI ZA KIMATAIFA ZA KUSIMAMIA HAKI ZA BINADAMU, BBC LONDON NA BALOZI MBALI MBALI
TAMKO RASMI CHADEMA UK
CHADEMA UK awali ya yote tunapenda kutoa pole kwa waTanzania na wapenzi wa CHADEMA waliopatwa na kukutwa na janga la kurushwa kwa bomu kwenye mkutano wa CHADEMA wa kuhitimisha shughuli za kampeni za uchaguzi wa madiwani huko Arusha. Tunatuma salam zetu kuwafariji wale wote walioguswa kwa namna moja ama nyingine katika jambo hili.
Kama waTanzania, tunapinga vikali na kukemea kitendo hichi kwa nguvu zetu zote. Mazingira na jinsi kitendo hichi kilivyotekelezwa tuna kila sababu ya kuamini kwamba hili ni tendo la kigaidi. Na kwa sababu hiyo ni jukumu la mamlaka (yaani serikali) na vyombo vyake vya dola kulinda na kuepusha matendo ya kigaidi kama haya.
CHADEMA UK awali ya yote tunapenda kutoa pole kwa waTanzania na wapenzi wa CHADEMA waliopatwa na kukutwa na janga la kurushwa kwa bomu kwenye mkutano wa CHADEMA wa kuhitimisha shughuli za kampeni za uchaguzi wa madiwani huko Arusha. Tunatuma salam zetu kuwafariji wale wote walioguswa kwa namna moja ama nyingine katika jambo hili.
Kama waTanzania, tunapinga vikali na kukemea kitendo hichi kwa nguvu zetu zote. Mazingira na jinsi kitendo hichi kilivyotekelezwa tuna kila sababu ya kuamini kwamba hili ni tendo la kigaidi. Na kwa sababu hiyo ni jukumu la mamlaka (yaani serikali) na vyombo vyake vya dola kulinda na kuepusha matendo ya kigaidi kama haya.
Subscribe to:
Posts (Atom)
